Bendera za nchi wanachama

Bendera za nchi wanachama

Sunday, December 21, 2014

Wasichana 100 waepuka tohara Tanzania


                                             
Umasikini na Ukeketeji watoto wa Kike

Zaidi ya wasichana mia moja wamehifadhiwa katika nyumba salama,baada ya kukimbia kuepuka tohara eneo la Kaskazini mwa Tanzania.Wasichana hao walilazimika kukwepa ibada hizo na hivyo kuondoka majumbani kwao kwa kuwa msimu umewadia na zoezi lazima litekelezwe.
Kwa muujibu wa desturi za serikali za mitaa,sheria ya kutahiri wanawake,ina maanisha ni kipindi cha mpito kwa binti kutoka kuwa msichana hadi mwanamke kamili,na hii inaashiria kwamba yuko tayari kwa kuolewa.
Wasicha mia moja kumi na nane kati yao wana umri wa miaka 10 hadi kumi na sita, wamehifadhiwa katika makazi salama na vituo vinavyoendeshwa na kanisa la Anglikan huko Mugumu, wilayani Serengeti.Rhobi Samwel ni mratibu wa mradi uitwao tunaweza ambao husghulika zaidi na kuupinga ukatili wa kijinsia.kwa muujibu Rhobi anaeleza kwamba mapema mwezi huu aliwaona mabinti hao wakiwa wamejikusanya kwenye vikundi,wengi wao wakiwa katika hali mbaya na hivyo kuwapeleka katika mazi salama.
Wasicha walio wengi wametokea wilayani Butiama,Tarime na Serengeti.miezi ya December na Januari ndio msimu wa tohara kwa wasichana na wavulana kwa mkoa wa Mara.viongozi wa maeneo husika wansema kwamba kupambana na kitu kinachoonekana kama ibada ya kitamaduni utamaduni ni suala nyeti na endelevu .
Sijali Nyambuche ni afisa wa polisi anayeshughulikia dawati la masuala ya jinsia na uangalizi wa wanawake na watoto huko Mugumu,Serengeti.Yeye anasema pamoja na masuala yanayohusiana na hatari za kiafya,jamii zimeendelea kushikilia msimamo wa kudumisha mila hiyo isiyo faa na hivyo kudumaza juhudi za kumaliza tohara mkoani humo.Sophia Simba, waziri wa maendeleo ya jinisa na watoto ana fafanua juu ya ukweli kuwa mara nyingi wasichana hukutwa wakiwa tayari wameshafanyiwa tohara ;
Kwa muujibu wa sheria ya makosa maalumu sheria ya mwaka 1998 ina kinza suala la tohara hutekelezwa kwa wasichana walio chini ya umri wa miaka 18,lakini sheria hiyo haitoi ulinzi ama tamko lolote mara baada ya wasichana hao wanapovuka kizingiti cha umri huo.adhabu kwa kosa la tohara ni kifungo cha miaka mitano hadi kumi na mitano .Ukatili huu umekuwa ukipungua tangu nchi ya Tanzania ilipopiga marufuku vitendo hivyo mnamo mwaka 1996 na hii imechangiwa na kampeni za kuijengea uwezo na kuielimisha jamii zilizokuwa zikiendeshwa na vikundi vya haki za binaadamu .



No comments:

Post a Comment